STORY

| No comment yet
Na Elisante Mkumbo na Victor Kinambile
Ili kuweza kuongeza mapato yatokananyo na utalii ,serekali imeombwa kuangalia uwezekano wa kuyafanyia matengenezo na kuya tangaza makumbusho mbalimbali nchini ili kuweza kuwavutia watalii waweze kufika kwa wingi.
Hayo yamesemwa na waandishi wa habari wa mikoa ya Singida na Tabora wakati walipotembelea makumbusho ya Tembe la David Livingston na nyumba ya mtemi Fundikira ambayo yapo mkoani Tabora wakiwa katika mafunzo ya siku nne juu ya uandishi wa mtandaao
Waandishi hao waligundua kusaulika kwa Tembe ambalo lilitumika kuwahifadhi watumwa kwaajili ya kuwasafirisha kwenda Bwagamoyo ambako walikuwa wakisafirishwa kwa mashuwa kwenda Zanziba hatimaye bara la Asia
Tembe hilo mwanzoni lilikandikwa kwa udogo juu ya paa lake na kuonyesha uhalisi ambapo liliwavutia watalii waliofika enzi hizo mpaka Wajerumani waliamua kulinunua kwa Rupia miamoja hamsini na kulihifadhi hadi walipojenga makao ya mkuu Kazahill (Tabora).
Kivutio kingine kilicho saulika na Wizara ya maliasi na utalii katika mji wa Tabora ni Jiwe lenye Ngoma, Bao,makalio na nyayo za watu wa kale.
Jiwe hilo ambalo lipo kando ya ngome ya mtemi Fundikira ambalo viongozi wengi wa serekali na mkoa wa mkoa wa Tabora wamekuwa wakipita na kuyaona bila kuya fayania matengenezo ambayo yangeweza kuwavutia watalii.

mwisho 

                                         Haya ni majengo ambayo yamesaulika kufanyiwa matengenezo

Post a Comment